Wakati mwingine umaskini au uhitaji wa mtu, hutokana na matokeo ya makosa anayofanya mtu mwenyewe, mhusika.
Kwakua huenda kukawa na furusa nyingi za kujikomboa, mtu anaziona, lakini mtu mwenyewe akawa hataki kuzitendea kazi, japokua hali yake ni duni, na yenye uhitaji mkubwa mno.
Basi umaskini na uhitaji unaweza kumuandama mtu wa namna hiyo kwa sababu ya ujinga wake mwenyewe, na wala mtu huyo asije mlaumu MUNGU.
baadhi ya mambo yanayoweza kumfanya mtu aendelee kuwa maskini na muhitaji ni kama haya yafuatayo_......
1_kuchagua kazi.
Kuna mtu hujifanya kuchagua kazi za kufanya, hutamani kufanya kazi kubwa kubwa, au zile zinazo onekana kua zenye kuheshimisha mbele za wengine, ili aonekane kua yupo juu, au ni mtu wa maana, hunyanyapaa sana kazi ndogondogo na kuwaona wanaozifanya kama hawana maana, au hawana thamani, au ni wajinga. Mtu wa namna hiyo hutamani mambo makubwa kabra ya wakati wake, hivyo husubiri sana kufikia viwango hivyo, bila mafanikio, hupoteza muda mwingi kwa kukaa na kungoja, na matokeo yake huambulia umaskini na uhitaji wa kutosha.
2_kuudharau mtaji mdogo.
Mtu mwingine hudharau pesa kidogo aliyonayo kwamba haiwezi kufanya biashara yoyote, hivyo huitumia hovyo hovyo na kuimaliza, huku akisubiria kupata pesa nyingi ili afanye biashara kubwa kubwa, huendelea kusubiria kupata mtaji mkubwa bila mafanikio yoyote, hatimae hali yake huzidi kuwa mbaya, hivyo umaskini na uhitaji wa kutosha huzidi kumuandama.
3_mtazamo wa kuajiriwa.
Mtu mwingine ameelekeza fikra zake kwenye kuajiriwa, na hana mtazamo wa kujiajiri mwenyewe.
Hivyo basi! Mtu wa namna hiyo huwa haisumbuwi akili yake kufikiria namna gani aweze kujiajiri, husubiria sana kupata ajira kutoka kwa watu wenye vipato, wenye nafasi zao, hungojea sana kwa muda mrefu bila mafanikio, mwishowe hali yake mtu wa namna hii huzidi kuwa mbaya, hivyo umaskini na uhitaji huzidi kumtesa mtu huyo.
4_uvivu.
Mtu mwinge anayo bahati ya kupendwa na watu, wanampatia kazi, ajira, lakini mtu huyo ni mvivu, hataki kujituma, hataki kufanya kazi kwa viwango vya kumridhisha tajiri yake.
Wakati mwingine hasara zinatokea kazini kwake kwa sababu ya uvivu unaopelekea utendaji kazi wake kuwa m'baya, hivyo matajiri kughaili kumuajiri kutokana na uvivu wake.
Ni mvivu hata kwenye kazi zake mwenyewe, hataki kufanya kazi kwa muda na wakati sahihi.
Mtu wa namna hiyo bila shaka atakua maskini na muhitaji wa kutupa.
5_matumizi zaidi ya kipato.
Matumizi zaidi ya kipato, yanaweza kumfanya mtu azidi kuwa maskini na muhitaji kila siku.
Kwa mfano kijana ana shilingi elfu kumi, anataka kuvaa 👖 jeans ya elfu kumi na nane, hivyo atakua mtumwa wa nguo, mpaka deni la elfu nane atakapo lipa.
Kwa mfano kuna mtu anapenda maisha ya mashindano katika matumizi, dhidi ya mtu wa wakaribu, bila kujua kua yule anaefanya nae mashindano anamzidi kipato, pia bila kuangalia kua matumizi anayofanya yatamuathiri kwa kiasi gani.
Pia mtu huyo anapenda starehe za anasa hata zina athiri kipato.
Hivyo huishi maisha ya umaskini na uhitaji kila siku.
Mtu yeyote anaweza kujikomboa dhidi ya umaskini na uhitaji, endapo tu ataamua kujikomboa.
Watu wengi wamekua wakidhani kua ni mpango wa mungu kuwa vile walivyo, kumbe inaweza ikawa sivyo, kwakua sio mpango wa MUNGU watu wawe maskini, bali WATU WA MUNGU WANA ANGAMIA KWA KUKOSA MAALIFA.
Badhi ya watu hudhani kua baraka za MUNGU huja kama miujiza, kumbe sivyo, baraka za MUNGU zitawafikia watu endapo watawajibika, watafanya kazi. Maana imeandikwa kua MUNGU atabariki kazi za mikono ya hao watakao fanya kazi, tena kwa bidii, na sio kwa ulegevu. Hivyo basi! Mtu yeyote asie fanya kazi, asitegemee kuziona baraka za MUNGU kwake.
Kwakua ahadi za MUNGU kumuinua mtu yeyote kiuchumi ni lazima zipitie kwenye KUFANYA KAZI.
haijalishi ni kazi ya namna gani, maadam iwe kazi halali, inatakiwa mtu anaetaka kubarikiwa aifanye, bila kujali kutazamwa na watu, ili mtu huyo abarikiwe, na atoke kwenye umaskini na uhitaji.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni