Alhamisi, 27 Aprili 2017

KUNA NGUVU MBILI ZA KIROHO KWENYE MAFANIKIO

mafanikio aliyo nayo mtu, yana tokana na nguvu za kiroho alizo nazo mtu.
Kila mtu anao upande mmoja wa kiroho kati ya mbili, ambapo ndipo huenda kuchukua mafanikio yake.

Kuna nguvu  aina mbili za kiroho, ambazo ili mtu afanikiwe katika maisha ya hapa duniani, ni lazima awe upande mmoja katka hizi mbili.
Nguvu zenyewe ni _MUNGU na SHETANI.
hizi nguvu zote zinatenda kazi, lakini hazipatani.
Hivyo mtu hawezi kufanikiwa Kama hayupo upande wowote mmoja wapo, na wala haiwezekani mtu kuwa pande zote mbili kwa wakati mmoja,  ni lazima mtu awe upande mmoja.
Kila nguvu inayo nafasi ya kutenda kazi kwa mtu alie upande huo, na alie tayari.

Kila upande wa nguvu hizi kunayo masharti, japokua masharti ya upande mmoja hayafanani na ya upande mwingine, ni tofauti kabisa.

Upande wa MUNGU masharti yake ni machache tu! Na tena yanafanana kwa watu wote wamuaminio, Kama ifuatavyo_
Usitende dhambi, usiache ibada yaani umuabudu MUNGU, usiwe mvivu yaani ufanye kazi zako na za MUNGU kwa bidii, usiache maombi, usisahau kutoa sadaka.
upande huu wa MUNGU hauna kafara, Kwani tayari MUNGU mwenyewe aliisha mtoa mwanae YESU KRISTO kuwa kafara pale msarabani kwa ajiri ya wote wamuaminio, hivyo hakuna sadaka ya damu (kafara).
Upande wa MUNGU upo msamaha, kwamba pindi mtu akisahau na kukosea/kutenda dhambi, akiomba msamaha/akitubu, MUNGU humsamehe mtu huyo, na wala hamfirisi/hamuondolei mafanikio aliyokua amempatia mtu huyo.

Upande wa SHETANI masharti yake sasa ni mengi mno, na hayafanani, mtu huyu anaweza kupewa masharti ya tofauti na ya mtu mwingine.
Kwa mfano_ huyu anaweza kuambiwa asiwe anakula nyama aina yoyote, asiwe anaoga ijumanne na ijumaa, asiwe anasafiri ijumanne,  hayo tu!
Lakini mtu mwingine akapewa masharti tofauti kama vile_ asiwe analala juu ya kitanda, asitembee na mwanamke nnje/tofauti na mkewe, asinywe pombe, nk, ili mradi tu masharti yao hayafanani,  hivyo kwa SHETANI masharti/miiko hua hayafanani, huyu hupewa tofauti na yule.
Kwa SHETANI kafara ni lazima, japokua mara nyingi kafara hutolewa kama adhabu, au hutolewa kama sehem ya matumizi ya utendaji kazi.
Kwa mfano_ mtu anaweza kutoa kafara ya damu ili mashetani wanywe wapate nguvu ya kumfanyia kazi yake ya mafanikio, kwakua damu ni Miongoni mwa vyakula pendwa vya kishetani.
Au kafara anaweza kutoa Kama adhabu ya makosa aliyo fanya, hasa kukiuka masharti aliyopewa.
Na kafara hazifanani, yaani kwa shetani mambo ni tofauti tofauti,  huyu anaweza kuambiwa atoe damu ya njiwa mweupe au mweusi au mwekundu,  mwingine akaambiwa atoe damu ya Kuku, au damu ya mbuzi, au damu ya n'gombe, au damu ya binadamu, hizo zote ni aina ya kafara.
Thamani ya damu inazidiana, na utendaji wa kazi zake nao unatofautiana, kwakua mafanikio yatakayokua kwa mtu alie toa kafara ya Kuku hayatakua sawa na yule alietoa kafara ya binadamu.

Kwa SHETANI hakuna msamaha, mtu akikosea ni adhabu tu! Tena wakati mwingine hata kunyan'ganywa yale mafanikio aliyokua kapewa.

Hivyo basi! Hakuna mtu anaeweza kufanikiwa kama hayupo upande wowote katika hizi mbili, ni lazima mtu awe upande wa MUNGU au upande wa SHETANI.
Hata Kama mtu ana kipaji, elimu, juhudi, bila kuwa na nguvu mojawapo ya kiroho katka hizi mbili, hawezi kufanikiwa.
Mafanikio yatokayo kwa MUNGU hayana majuto, lakini mafanikio yatokayo kwa SHETANI yana majuto makubwa Sana.
Hivyo basi! Ni vema mtu kumngoja MUNGU hata utakapofika wakati wake wa kubarikiwa na kuingia kwenye mafanikio, kuliko kufanya haraka kuyakimbilia mafanikio ya SHETANI ambayo huleta majuto, na mwisho wake hua ni m'baya zaidi.

             (Elisha Emmanuel rutale)

Jumatano, 26 Aprili 2017

YALIYO MPATA MWANAMKE MPUMBAVU :

Hiki kisa unaweza Kusema ni hadithi tu! Lakini sivyo, bali ni kisa cha Kweli. Soma kwa makini, na ujifunze kutokana na makosa aliyoyafanya binti/mwanamke Kama  wewe.

Kijana alikua muuza magazeti ya kutembeza mkononi (machinga).
Kwakweli hali yake ya uchumi haikuwa nzuri, Kwani mshahara wake ulitokana na idadi ya mauzo ambayo angeuza kwa siku,  kipato hicho ndicho kilimuwezesha kupata mahitaji yake ya kila siku, pia kulipia kodi ya pango/nyumba aliyokua akiishi. Hakika kijana huyu alikua na hali ngumu, kwani chumbani mwake kulikua kuna ndoo mbili ndogo, moja ya kuogea, na nyingine maji ya kunywa, na kikombe kimoja tu!
Kijana huyu alikua na kitanda kisichokua na godoro, hivyo alitandika mkeka kwenye chaga, na usingizi ulikua unapita, na maisha yalikua yanaendelea.

Siku moja kijana akiwa kwenye harakati zake za kuuza magazeti, alimuona binti akiwa amesimama, akamsogelea,,,,,
Kijana,,,,,,,,,, habari yako,
nzuri,,,,,,,,,,,,,,,, aliitikia binti.
Kijana,,,,,,,,,,,,,Mbona umesimama hapa kwa muda  nini shida?
Aah! Kuna mtu namsubiria,,,,,,,,,,alijibu binti.
Kijana,,,,,,,,,,,,,,,,Okay, ninaweza kujua wapi unapatikana ili baada ya kazi nikutafute, tuzungumze machache?
Binti,,,,,,,,,,,,,,,nisikudanganye, sio rahisi kunipata nyumbani, kwani wazazi wangu ni wakali sana, rabda nitakuja huku tena kesho tutaonana tutaongea.
Kijana,,,,,,,,,,,,,,,Pouwa! Mida gani?
Mida kama hiihiii!nitakuja,,,,,,,,,,,,,,alijibu binti huku akielekea kwenda kukutana na mtu aliekua amemsubiria, ambae alionekana ni mama wa umri kama mama yake.
Waliondoka, na kijana aliendelea na kazi yake ya kukata mitaa, kutafuta wateja wa magazeti yake 
Kesho ilifika, na binti kwa uaminifu kabisa alifika sehem ile mida ile ile waliyo patana,  muda kidogo kijana nae akawasiri.
Mambo,,,,,,,,,,,,kijana alimsalimia binti.
Pouwa,,,,,,,,,,,binti aliitikia.
Da! Mimi nilidhani hautakuja, nilijua umenidanganya, maana watoto wa mjini wengi waongoo!!!,,,,,,,,,,,aliongea kijana yule, huku akimpa ishara ya kua waondoke maeneo yale.
Binti,,,,,,,,,,,,,,,,kwa nini nikudanganye, kwa faida gani, kama ningerkua siji ningekuambia tu kwamba sitokuja.
Walielekea sehem kulipokua kunauzwa vinywaji, wakachukua viti na kuanza mazungumzo yao. Kijana akamuelekeza binti anapoishi, akampa na ratiba ya mida gani huwa anakua amekwisha rudi nyumbani ili binti aweze kumtembelea. Binti alimsihi kijana yule kwamba endapo atakua akienda kwake asiwe anamchelewesha kurudi nyumbani, Kwani wazazi wake ni wakali mno.
Kijana alimuahidi kufanya sawa na binti alivyo sema.

Wakaanza Mahusiano ya kimapenzi, wakapendana vilivyo, wala binti hakuona hali duni ya uchumi wa mpenzi wake kua ni kitu, japokua binti kwao mambo yalikua safi, na baba yake binti alikua mfanyakazi mstaafu, hivyo kwao na binti hakukua na shida ndogo ndogo, lakini tayari alikua amekolea kwa kijana maskini, muuza magazeti, mwenye kitanda kisichokua hata na godoro.
Mapenzi yaliendelea, lakini waswahili wanasema _PENZI NI KIKOHOZI HALIFICHIKI.
Tayari wazazi wa binti wakagundua kua binti yao anamimba. Tayari wakamfukuza nyumbani, binti akakimbilia kwa mpenzi wake, maisha ya mme na mke.
Kijana hakuwa na sufuria ya kupikia wala bakuli wala sahani wala mwiko,  ilibidi waanze kuishi kwa kula mgahawani, baada ya siku chache walipata vyombo vya kuanzia maisha vile vya mhim kwanza, maisha yakaanza kusonga mbele.

Kijana aliendelea na kazi yake ya kuuza magazeti.
Siku moja kijana anafika ofsini kwao, anakutana na msiba, nani?, bossi wake amepata ajali na kupoteza maisha.
Wakafanya msiba, hatimae msiba ukaisha.
Sasa ofisi haina msimamizi, bossi, hivyo ikabidi mwenye kuihitaji nafasi ile ajaze fom, Miongoni mwa wachache walio jaza fom, kijana yule baba harusi mpya akaibuka ushindi na kua bossi. Furaha ya ajabu aliyo fika nayo nyumbani kijana yule, na kumhadithia mkewe jinsi ambavyo MUNGU amewakumbuka na wao.

Sasa maisha yalianza kubadilika, kijana akanunua vitu vyote mhim vya ndani, tayar nyumba waliyokuwa wakikaa ikawa haina kiwango chao, wakatafuta nyumba nzuri ya gharama, yenye hadhi, yenye usalama wa kutosha, maisha yakawa burudaani!!!
Kutokana na namna ambavyo kijana allipenda kazi yake, na kuifanya kwa ufanisi, alimpata tena nafasi ya kuwa mkurugenzi wa gazeti ya FEMA mkoa, hivyo yeye ndie aliekua mpokeaji, msambazaji, na msimamizi wa gazeti la FEMA katka shule zote za secondary mkoa wote.
Basi posho ikaongezeka, kipato kikapanda, ofsi yake ghorofa ya pili juu! Mambo yakawa good.

Kijana akaona sasa anapesa, hivyo ni vema amuwezeshe na mkewe, ili nae awe na kitu/kazi ya kufanya.
Mwanamke akaitaji apelekwe veta ili ajifundishe ufundi,  veta akapelekwa,  akawa fundi mzuri Sana wa cherehani.
Kijana akaona si vema mkewe afanye kazi moja tu ya ufundi, akamfungulia duka la nguo spesho, nnje mbele ya duka lake mwanamke akaweka cherehani, akawa akishona, na kuuza duka.
Siku si nyingi mwanamke akasema yeye kazi ya dukani na kushona hawezi, bora akae nyumbani alee mwenyewe watoto wake, kwani tayari walikua wameisha pata watoto wawili ambao walitafuta yaya akawa akibakia nao nyumbani 
Mwanamme akasema sawa mke wangu, wewe ndie mke wangu kipenzi, tulieanza wote maisha ya taabu, chochote utakacho nitakufanyia.
Mwanamke akasema nataka nikae nyumbani niwe nauza maji baridi (kandoro) na ice cream, hivyo ninunulie Friji na friza,  kijana akasema kwa hilo ondoa Shaka mke wangu nitafanya.
Mwanamke akarudi nyumbani akaanza kuuza maji na ice cream, kule dukani wakaweka mfanya kazi/ msaidizi,  ambae pia alikua fundi ili kuitumia cherehani.
Mwanamke kafanya ile kazi, mara kazi ile nayo ikawa ngumu,  akamwambia mmewe, hii kazi imenishinda ninachoka Sana mgongo kwa ajiri ya kukaa muda mrefu kufunga maji na ice cream, naomba tu niiache.
Mwanamme akasema ondoa Shaka mke wangu, wewe ndio mke wangu, na mama watoto wangu, mimi sjashindwa kuwatunza, na kumbuka tuliko toka na tulipo kwa sasa, hebu tulia lea/hudumia watoto wetu wafrahi na mama yao.
Mwanamke akawa mama wa nyumbani.
lakini kumbuka kua ukiwa hauna kazi, shetani nae atakupa kazi ya kufanya.
Mwanamke yule akaanza tabia za uzinzi/umalaya, ikawa mme wake akiondoka kwenda kazini, na yeye anaanza ujinga wake wa uzinzi.
Mwanamme akalijua hilo, kwakua alikua anampenda, alivyokua akikumbuka walipotoka kwenye hali mbaya ya uchumi, hakupenda kuchukua maamuzi ya haraka, bali aliendelea kuvumilia, huku akizidi kufanya uchunguzi, na kutafuta ushahidi wa yale anayo fanya mkewe,  ili pindi atakapo fanya maamuzi kusiwepo lawama.
Mwanamke aliendelea na tabia yake ya uzinzi, hadi ilipofikia kukosa heshima kwa mmumewe.
Vituko vikawa haviishi ndani, mwanamke anamuinukia mmewe kwa matusi na kashifa, mara ooh! Mmewe hajui mapenzi, kwamba wapo wanaume wanao jua mapenzi na wala sio mmewe, sms zinaingia holela, simu zinapigwa bila mpangilio kutoka kwa wapenzi wake, mbele ya mmewe.
Kwakweli Vituko vilizidi hadi mwanamme akashindwa kuvumilia.
Siku moja nilikwenda kwao, kwakua yule kijana alikua rafiki yangu Sana, siku hiyo nilifika Kama kawaida sehemu ikiwa kwa rafiki yako wa kweli, unakua hauna mashaka ya mazingira, nikafika nasukuma mlango wa sebuleni ili niingie, ile tu naingia nilikutana na kituko cha ajabu pale sebuleni alichokua akikifanya yule Shemeji yangu,,,,,,,,

        Nini nilicho kiona dhidi ya mwanamke yule?
               Usikose kuwa nami pale nitakapo kuletea mkasa huu kwa awamu ya pili.

Jumatatu, 24 Aprili 2017

HASARA ZA KIMAPENZI :

mapenzi ni kitu cha kuvutia na cha kupendeza, pale tu ambapo wapendanao walifanya maamuzi sahihi na yasiyokua na majuto.
Lakini mapenzi yana maumivu makubwa yanayo ambatana na hasara za mipango ya kimaisha, pale tu wapendanao wanapo anza kutofautiana.
Kuna watu wengi ambao mipango yao mingi na mikubwa imeharibika kwa sababu ya hasara za kimapenzi.
Kuna watu wamefirisika walikua na biashara kubwa kubwa, kuna watu wamepoteza hata nafasi zao za kazi kwa sababu ya hasara za kimapenzi.
Upo uwezekano mkubwa hata wa mtu kuukosa ufalme wa MUNGU, kwa sababu tu amevurugwa na mpenzi wake.

Kuna Ndugu mmoja mkoa (nauhifadhi) yeye alikua mfanya biashara mkubwa tu, lakini walipo anza kutofautiana na mkewe, mambo yalianza kuharibika.
Ilibainika kua mwanamke alikua akichota pesa kwa Siri na hatimae kwenda kujenga nyumbani kwao.
kwakua Mali ile waliitafuta wote, ilikua ngumu kwa Jamaa kumtoa kwenye biashara mkewe. Hivyo basi ilikua ni mashambulizi, kila mmoja akawa akiuza anachukua chake, hatimae biashara ikafika ukingoni, na Mahusiano ya mapenzi yao yakaishia Hapo.

Kuna binti mmoja alijinyonga kwa sababu ya mapenzi. Binti huyo alikua na Mahusiano na kijana ambae hakua mkweli, Kwani tayari kijana Yule alikua anamwanamke alimuacha kijijini kwao.
Kijana Yule alikwenda mjini kutafuta maisha, ndipo alipo kutana na yule binti na kuanza Mahusiano kisha wakaanza kuishi kama mke na mme.
Maisha yalikua mazuri kiasi kwamba Yule kijana alikua anakwenda kuchukua biashara nnje ya nnchi, na nguvu kubwa ya mtaji ilikua ya Yule binti, Kwani binti Yule alikua mfanyakazi kwenye kiwanda cha vinywaji, kitengo kikubwa tu cha mshahara wa kutosha.
Mapenzi yao yalikua moto moto, kwakua kila mmoja wao alijitahidi kumuonyesha mwenzie mambo mapya ya kimapenzi kila siku.
Binti alimpeleka kijana nyumbani kwao, na hatimae wakaowana kabisaa! Lakini kijana Yule alikua amekwisha oa mwanamke kijijini kwao, tena kwa ndoa halali ya kanisani. Na tena mkewe huyo alikuwa na watoto wawili.
Baada ya taalifa kufika kijijini kwao na kijana kua kwa sasa mambo yake ya kifedha yako vizuri, ilibidi mkewe huyo wa kijijini aende kumtafuta mmewe, na hatimae alimpata, na mmewe ilibidi amkaribishe nyumbani kwani hakuona vyema kuwakataa watoto wake ambao ni damu yake mwenyewe.
Jambo hilo likawa jipya na geni machoni pa binti Yule ambae ni mkewe mdogo wa mjini kwakua hakulijua toka mwanzo, yeye alijua kua yuko peke yake.
Kutokana na jinsi alivyo kua akiheshimika pale mtaani, na kazini kwake, na jinsi alivyo mpokea Yule kijana toka kijijini, na jinsi walivyokua wakishirikiana, na mipango na ahadi nyingi walizokua wameweka mbele yao, Yule binti alikosa uvumilivu, hatimae akaamua kujinyonga.
Ninayo mifano/visa vingi tu vya kuonyesha athari zinazo weza kumpata mtu endapo tu hakuwa makini kwenye maamuzi ya kuchagua mpenzi anaefaa.
Lakini ukweli ni kwamba zipo athari kubwa za kimapenzi zinazo weza kumpata mtu asipokua makini mwanzo.
Hauwezi kuwa baba wa familia bora Kama utakosea kwenye maamuzi ya kuchagua.
Hauwezi kuwa mama wa familia bora, kama utakosea kwenye maamuzi kuchagua.
Hauwezi kuwa na familia yenye malezi bora, kama ulikosea kwenye maamuzi ya awali.
Jamii inayo kuzunguuka, majirani, rafiki zako, wafanyakazi wenzio, hawawezi kukuheshim Kama haukuwa makini kwenye maamuzi yako ya awali ya kuowa/kuolewa, kwakua ili nyumba yako iwe imara ni lazima uwe makini Sana kwenye ujenzi wa msingi, lakini endapo tu utaboronga kwenye ujenzi wa msingi, basi nyumba yako /jengo,  haitakua imara, haitadumu muda mrefu, ipo sku itakuangukia na kukuaibisha.

        Uwe makini Sana unapofikia wakati wa kufanya maamuzi ya kuchagua mke/mme, kwakua ukikosea Hapo, umekosa, furaha, Heshima, pesa, afya, ufalme wa MUNGU, nk.

Jumamosi, 22 Aprili 2017

Rafiki wa kweli ni yupi?

Rafiki ndie mtu pekee wa karibu.
Rafiki ndie msiri wa rafiki yake.
Ndio maana ni vema kuwa makini Sana wakati wa kuchagua rafiki, kwakua rafiki anaweza kukusaidia, pia rafiki anaweza kukuangamiza.
Unaweza Kua umeoa lakini mkeo akawa mkeo tu, na asiwe na sifa ya kuwa rafiki yako.
Unaweza kua umeolewa lakini mmeo akabakia kuwa mmeo tu, na asiwe na sifa ya kuwa rafiki yako   Unaweza kubadilika kitabia au ukawa mwema, au ukawa m'baya kutokana na rafiki ulie nae.
Sio kila mtu alie karibu nawe anastahili kuwa rafiki yako, kwakua rafiki ni nafasi kubwa, na ya pekee ambayo kabla haujampa mtu nafasi hiyo unapaswa kumchunguza Kama anastahili kupewa, kwakua ndoa nyingi zimevunjika Kwasababu ya rafiki. Biashara nyingi zimekata kwa sababu ya rafiki. Hata kuna watu wameuwawa na marafiki walio waamini kabisa.
RAFIKI WA KWELI lazima ujue viwango vyake vya upendo Kwako. Ujue viwango vyake vya hekima na busara. Ujue kua kwake yapo mambo mazuri ambayo unaweza kijifunza, asiwe mwenye mambo ambayo ukiiga yatakuangamiza.
KWA MFANO_ akina Dada, rafiki yako akiwa kahaba/changudoa ni lazima nawewe utakua hivyo, kwa sababu upo muunganiko wa ushirikiano kwenye ulimwengu wa roho ambao lazima utajidhihirisha katika mwili.
MFANO_ akina kaka, kama rafiki yako akiwa teja/mwizi/mlevi/mvivu/nk, lazima na wewe utakua na tabia Kama zile, kwakua Miongoni mwa mambo ambayo marafiki hufanana ni pamoja na kuwaza, kula, kustarehe, nk.
Jambo la kufanya kabla hauja fanya maamuzi ya Yule kuwa rafiki yako, ni lazima ujue kua Je! Kuna mambo mema mazuri ambayo anayo rafiki yangu mtarajiwa, ambayo nitajifunza kutoka kwake? Je! Ni mazuri Kweli?
Na Kama rafiki yako mtarajiwa Hana sifa njema basi achana nae, pia nafasi ya urafiki usimpatie, kwakua ni HELI UWE PEKE YAKO, KULIKO KUWA NA RAFIKI WA HASARA NA WA KUKUANGAMIZA. rafiki mnafiki.

Tabia zitakazo kufanya umfaham mpenzi asie kufaa.

Watu wengi wamekua wakiteswa/wakiteseka na mapenzi, wengine wamesusa na kuapa kua hawatapenda tena! Lakini si Kweli Kwamba kufanya hivyo ndio suruhu ya maumivu yaliyo wahi kuwapata.
Kwa sasa nataka niwatahadharishe vijana wa kiume, kuhusu tabia ambazo zinaweza kuwasaidia kujua kama mpenzi alie nae hamfai endapo atamuona ana tabia Miongoni mwa hizi zifuatazo.
1_umekaa na mpenzi wako mahali frani, tangu mlipo kutana mpaka mnaagana vidole vyake havitulii kwenye cm, yeye ni kupokea sms na kutuma sms, na ukimtazama kwa makini unaona yuko busy na cm kuliko kua busy na wewe, ujue huyo hampo nae kwenye mapenzi ya Kweli, huenda wewe ni wa ziada.
2_hakupigii cm mpaka umpigie wewe, hata ukimtumia Salio hua hakupigii cm, mpaka wewe umpigie, ujue huyo hampo nae kwenye mapenzi ya Kweli, huenda wewe ni ziada.
3_anataka matumizi Kwako ya juu kuliko anavyo kiona kipato chako, sku usipo mtimizia mahitaji yake ya kipesa, anakususa kwa siku kadhaaa.
4_Pindi anapokukosea haombi msamaha, hapendi kuwa chini yako.
5_hapendi ushauri wako, na wala hajawahi kukuomba ushauri hata siku moja.
6_anapenda kukosoa maisha ya wengine, anajiona yeye ni bora kuliko watu wengine.
7_hua ukimpeleka nyumbani unapoishi lazima akosoe jitihada za mandhari yako, na kukuvunja moyo kwa kile ulicho jitahidi kufanya kadri ya uwezo wako.
8_hapendi kukushirikisha mipango yake ya kiuchumi, wakati mwingine hataki ujue kabisa!
9_hapendi uwe unakwenda nyumbani kwake, kwao.
10_hauna uhuru na cm yake huenda hata passward ya cm yake hauijui.
KAMA UTAONA TABIA HIZI KWA MPENZI WAKO BASI CHUKUA HATUA, KWAKUA HIZO NI DALILI TOSHA ZA KUJUA KUA HUYO NI MPENZI WAKO WA KWELI, AU NI JAMBAZI NA TAPELI LA KIMAPENZI.
           hii inawahusu akina kaka kuwafaham wapenzi wao.

Bidii bila MUNGU ni bure

Watu wengi wamejitahidi kutafuta maisha kwa bidii zao zote, lakini walio wengi wamekua wanatumia nguvu nyingi, mafanikio yanakua kidogo.
Kwanini?....
Kwasababu kila mafanikio yana nguvu ya ziada ya kiroho, ambayo bila hiyo hakuna mafanikio.
Kwa wasomaji wa biblia watakumbuka kisa cha daudi na goliathi, daudi hakutumia nguvu nyingi Kumuangusha goliathi, bali alitumia jiwe moja tu! Miongoni mwa mawe matano aliyo kua nayo.
Kwa nini?..
Kwa sababu alikua na nguvu nyingine ya kiroho.
Walikuwepo watu mastadi wa Vita, na wenye zana zote za kivita za enzi zile, lakini hawakuweza kumpiga goliathi, kwa sababu hawakua na nguvu za kiroho ndani yao, bali walizitumainia nguvu/maalifa/akili zao ambazo hazikuwasaidia.
Hivyo basi mafanikio hayatamfikia mtu Kwa sababu tu anabidii Sana, bali kwa sababu ndani ya bidii zake Iko nguvu ya MUNGU itendayo kazi, ambayo ndiyo hasa itakayo mfanya mtu atoke chini kwenda juu.
Hivyo basi bidii bila MUNGU ni kujichosha kusiko na mafanikio.